KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday 14 May 2016

WAITAKA UDART KUTOA KADI ZA USAFIRI HARAKA ILI KUZUIA MSONGAMANO WA KUNUNUA TIKETI DIRISHANI



BAADHI ya abiria wanaotumia usafiri wa mradi wa mabasi yaendayo haraka, wamesikititishwa na ucheleweshaji wa uzwaji wa kadi za kutunzia nauli kila wanapotaka kusafiri katika mabasi hayo.
Baada ya uzinduzi wa mabasi hayo Mei 10 mwaka huu, abiria hao waliahidiwa na maofisa waliyoko kwenye vituo vya mabasi hayo kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu atumizi ya magari hayo, kwamba wangeanza kuuziwa kadi hizo kuanzia Mei 12 mwaka huu.
Wakizungumza jijini Dar es Salaam jana, Abiria hao, walisema walifika katika vituo hivyo asubuhi ili kujipatia kadi hizo lakini wakazikosa kwa madai kuwa bado utaratibu wake unaandaliwa.
Dorcas James, alisema wamefikia hatua hiyo kwa vile wanaamini kumiliki kadi hiyo kutaondoa usumbufu kwa abiria anayetaka kusafiri,  kwani atakapofika kituoni hatapanga foleni ya kununua tiketi.
Hata hivyo, alisema kuchelewa kuuzwa kwa kadi hizo kuna tiashaka kwami maofisa waliyokuwa katika baadhi ya vituo hivyo walishindwa kutowa majibu ya kuridhisha kwa abiria kuhusu kuchelewa huko.

“Unajua kuchelewa kuuzwa kwa kadi hizo kunaonesha jinsi waendeshaji wa mradi huo walivyokuwa hawajajiandaa kuanza kwake,”alisema Dorcas.
Alisema, pamoja na kuwepo utaratibu mfumo mwingine wa tiketi, anaamini siku ya Mei 16 mwaka huu utakapoanza utaratibu wa malipo kutakuwa na vurugu kutokana na wingi wa abiria watakaokusanyika kwa ajili ya kusafiri.
Naye James Charles, alisema mwiitikio wa abiria ni mkubwa kwa hivyo utoaji wa tiketi kwa siku hiyo hiyo ya safari utaleta usumbufu kwani unaweza hata kuchelewesha safari.
“Kingine magari bado hayaoneshi ruti hivyo wakati mwingine kuwafanya abiria kupanda gari lolote na kujikuta akianza kuhangaika mara anapojikuta amejaribu kuingia kwenye gari ambalo siyo lake,”alisema Charles.
Kwa nyakati tofauti mofisa waliyoko kwenye vituo bila kutaja majina yao walisema awali walitoa ahadi hiyo ya kuanza kuuzwa kadi hizo kutokana na maaelekezo ya viongozi wao.
Walisema, baada ya kukwama kuuzwa kuanzia juzi, viongozi wao wamesema wanalishugulikia na kuanzia sasa zitaanza kuuzwa.

No comments:

Post a Comment