KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday 17 May 2016

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MATUMIZI HOLELA YA RAMANI YA TANZANIA ILI KUZUIYA UPOTOSHAJI



WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, WILLIAM LUKUVI

SERIKALI imepiga marufuku matumizi ya Ramani ya Tanzania baada ya kubaini upotoshwaji wa mipaka ya nchi jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa nchi.
Hatua hiyo inakuja baada ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kubaini matumizi ya ramani ya Tanzania kwenye majarida, magazeti na hata luninga inayopotosha mpaka kwamba sehemu ya ziwa Nyasa ikionesha kuwa mpaka wake unapita pembezoni mwa ziwa.
Katika mazungumzo yake na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani, Justo Lyamuya, alisema ili kuepusha upotoshaji huo wa mipaka ya nchi serikali inashauri kwamba kila mmoja lazima atumie ramani sahihi.
Alisema, kuwa kitendo chochote cha kuchapisha ramani yenye makosa kwa makusudi au bila kujua kwa kutumia vyanzo visivyo rasmi ni kosa kwa mujibu wa sheria za nchi hivyo atakaye kaidi baada ya kuelimishwa anaweza kuchukuliwa hatua.
Lyamuya, aliwataka watumiaji wa ramani kutambuwa kuwa ramani sahihi ya Tanzania inatakiwa kuonesha mpaka kwa sehemu ya maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa ukipita katikati ya maziwa hayo na siyo vinginevyo.
Aidha, wadau wote wanapaswa kutambua kuwa Idara ya Upimaji na Ramani ndiyo yenye mamlaka ya kuandaa, kuchapisha, kutunza na kusambaza ramani zote nchini, ambayo ipo tayari kutoa ramani kwa matumizi yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kutoa elimu na ushauri kuhusu usahihi wa ramani kabla ya kuitumia.
 “Kutumia vyanzo visivyo rasmi ni kosa kwa mujibu wa mamlaka (Instrumen) ya Waziri aliyepewa dhamana ya kusimamia sekta ya aardhi ikiwemo masuala ya upimaji ramani,
“Jambo hili likiachwa liendelee kuna hatari nchi ikaingia kwenye mgogoro kwani kuna baadhi ya nchi zimeingia kwenye migogoro chanzo ikiwa na kugombea mipaka,”alisema Lyamuya.
 “Napenda kuchukuwa fursa hii kuwatangazia Watanzania na wadau wote hapa nchini kuwa ramani sahihi ya Tanzania inayoonesha mpaka wa Tanzania ni hii ambayo kwa sehemu ya ziwa Nyasa mpaka wake unapita katikati ya ziwa hilo,”alisema Lyamuya.
Hata hivyo, Lyamuya, alisema kwa yeyote nahitaji ramani hiyo sahihi kwa ajili ya matumizi afike katika duka la wizara hiyo lililoko Temeke, mahali palipokuwa Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
Alisema, vile vile ramani hiyo pia inapatikana katika tovuti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa anwani;www.ardhi.go.tz
Akizungumzia uasalama wa mipaka ya iliyoko baharini, Lyamuya, alisema hadi sasa mipaka yote haina matatizo nchi zote zinazopakana na Tanzania zinaheshimu makubaliano saini.   

No comments:

Post a Comment