ASKOFU
Mkuu wa Kanisa la The Evangelistic Assemblies of God Tanzania
(EAGT), Dk Brown Mwakipesile amewataka wa umini wa kanisa hilo
kudumisha amani, ambayo itawafanya waweze kuendesha ibada katika hali ya
mshikamano.
Hayo
aliyasema juzi, wakati alipoongoza viongozi na washirika wa makanisa ya
EAGT katika ibada maalum ya kumtambulisha kwa wa umini, iliyofanyika katika
Ukumbi wa PTA uliopo kwenye viwanja vya maonesho ya Kimataifa ya biashara ya
Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Askofu
Dk. Mwakipesile alishika nafasi hiyo Oktoba mwaka jana baada ya Agosti
29 2013, kufariki Mkuu wa Kanisa hilo, Askofu Dk. Moses Kulola.
Ibada
hiyo ilihudhuriwa, baadhi ya viongozi na washirika wa makanisa ya EAGT
kutoka majimbo ya Kinondoni, Temeke na Pwani, ambapo Dk.Mwakipesile aliwataka
waumini wa kanisa hilo kuwa na moyo wa kujitolea kwa ajli ya kununua viwanja vya kujenga makanis
Alisema
makanisa yakiongezwa na waumini wakishiriki katika ibada wataweza kujua
mahitaji yao makubwa ambayo yanahitajika kupatiwa ufumbuzi wa pamoja ikiwa ni
kati ya viongozi na waumini.
“Watu
wasome,wazalishe ili kizazi kinachokuja kiweze kufundishwa Injili, tukitaka
tushinde lazima tuhubiri Injili,”alisema Askofu Mwakipasile nakuongeza;
“Mimi
wakati nachaguliwa sikuwa na wazo la kuchaguliwa, tangu nimeanza kumtumikia
mungu nimeanza uongozi ngazi za chini,kitu ambacho nimeweza kujifunza kwa
marehemu Kulola ni kujiuliza wapo wangapi wenye mfano kama wake yeye mwenye
uchungu nikabaki tuu kumuombea hivyo basi nawasisitiza tuitangazeni
Injili,”alisema Dk. Mwakipasile.
No comments:
Post a Comment