KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 17 April 2015

BAWACHA WATOA MSAADA WA VYAKULA



BARAZA la Wanawake la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), Jimbo la Ukonga, limetoa msaada wa vyakula kwa vikongwe na wajane ambao wanahitaji kusaidiwa kwa hali na mali kutokana mazingira magumu wanayoishi.

Akizugumza wakati wa makabidhiano hayo yaliyofanyika Mtaa wa Kiyombo Kata ya Kitunda wilayani Ilala jijini Dar es Salaam, Katibu wa Bawacha Asia Msangi, ambaye ndiye mfadhili mkuu wa misaada hiyo, alisema kuwa vikongwe na wajane ni kundi ambalo serikali imelisahau kitendo ambacho kinawafanya wajisikie kama vile hawana haki ya kuishi katika nchi yao.

Alisema Bawacha, limefikia hatua hiyo, baada ya kubaini miongoni mwa watu hao wamo walioshindwa kupata huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo watoto wa familia hizo kukosa elimu.

“Kwa mfano kundi hili la vikongwe, hawa ni watu ambao wamelitumikia taifa kwa uadilifu wakati wa tumishi wao sasa sio vizuri kwa serikali ikawasahu,”alisema.

Asia, alisema Chadema ni chama makini, akibainisha kuwa utoaji huo wa misaada haukuanza mwaka huu bali ni mwendelezo nadni ya kipndichote cha miaka mitano.

Aliyekuwa Katibu wa Jimbo hilo Juma Mwipopo, aliweleza vikongo na wajane hao kuwa matatizo yao yametokana na serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambayo viongozi wake wameweka ubinafsi mbele.

Alisema kama wananchi wanahitaji mabadiliko ni vema wakaiondoa CCM katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanika Oktoba mwaka huu.

“Wazee wangu tambueni kuwa fedha zipo zinatengwa na zinaletwa katika kata yenu, lakini uchoyo na kukosa uadilifu kwa viongozi waliyoko madarakani kutojali watu wenye mahitaji maalum hali inayoifanya nchi ionekane haipendi kundi hilo,”alisema Mwipopo.

Mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Staf Sajent Machael Marwa, alisema wanakishukuru Chadema kwa kuwapatia msaada huo kwa vile haujatokea kwa vikongwe wa kata hiyo kupewa misada.

“Huu msaada ni mkubwa kwa kuwa wako vigogo wameshindwa kufanya hivyo katika maisha yao sasa kwani sisi tusishukuru tunawomba wengine nao wapige mfano kama huu wa Chadema.

Naye Wegesa Borogo, amabye ni mjane alisema kuwa wanakiomba chama hicho kuharakisha mpango wake wa kuanzishia Saccos kwani anaamini itawasaidia katika kujiletea maendeleo katika familia zao.

No comments:

Post a Comment