KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 17 April 2015

MPINGA ATOA ONYO KWA WAZUSHI MITANDAONI



KAMANDA wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mohamed Mpinga, ametoa onyo kwamba Jeshi la Polisi nchini halitasita kuwakamata watu wanaotoa taarifa za ajali za uongo katika mitandao ya kijamii wakionyesha aina ya basi na kudai kuwa yamepata ajali.

Mpinga, alitoa kauli hiyo wakati alipozungumza na wandishi wa habari, kuhusu malalamiko kutoka Kampuni ya Dar Express kwamba katika kipindi cha wiki mabasi ya kampuni hiyo yamehusishwa mara nne kwenye mitandao ya kijamii kuwa yamepata ajali huku taarifa hizo si za kweli.

Alisema, baada yakupokea taarifa hizo za uzushi, tayari wamekwishaanza uchunguzi ili kuwabaini watu hao ambao hadi hivi sasa haileweki wana lengo gani.

“Ni kweli picha za ajali za mabasi ya Dar Express zilikuwepo zilionekana kweye mitandao ya kijamii hali iliyofanya wananchi kutoka pembe zote za nchi,”alisema.

Mpinga, alisema vitendo vinavyofanywa na watu hao ni ukiukwaji wa sheria kwa vile wanajua fika kuwa hakuna gari la kampuni hiyo lililopata ajali.

Alisema watu hao katika kutekeleza uzembe wao wamekuwa wakiweka katika mitandao picha za mabasi ambayo yalipata ajali niaka sita iliyopita.

“Hii ni hatari wamekuwa wakizusha hofu katika familia za jamaa ambao walikuwa ndugu zao wako safarini na wapo watu waliokumbwa na shinikizo la damu kutokana na taarifa hizo ni waombe watanzania kuwa waitumie mitandao hiyo kwa lengo la kujielimisha,”alisema.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Dar Express, Yudika Mremi, amewaomba radhi abiria wake na kwamba hakuna basi la kampuni hiyo lililopata ajali hivi karibuni.

Alisema kutokana na taarifa hizo, uongozi wa kampuni hiyo tayari umekwishatoa taarifa polisi, ili wafanye uchunguzi wao na hatmaye kubaini malengo ya watu wanaotoa za upotoshaji.

Mremi, ameitaka jamii kutoa ushirikiano katika kuwasaka watu hao ambao katika nia yao ningine ni kuvuruga biashara za wafanyabiashara wengine jambo ambalo halitawaletea manufaa katika maisha yao.

No comments:

Post a Comment