MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imemhukumu
kifungo cha miaka mitatu jela, mpwa wa Mwekahazina wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM), Mkoa wa Kigoma, Rajabu Maranda, Farijala Hussein baada ya kutiwa hatiani
kwa makosa sita likiwamo la kujipatia sh. milioni 455 kwa udanganyifu.
Hukumu hiyo iliyochukua saa tatu ilitolewa
jana na jopo la mahakimu watatu ambao ni Francis Kabwe, Projestus Kahyoza na
Panela Mazengo.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mazengo
alisema mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka mitatu jela kwa kila kosa.
Hata hivyo, adhabu hizo zitakwenda
sambamba, hivyo mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka mitatu jela.
Mbali na hukumu hiyo, hakimu huyo
alimtaka mshtakiwa huyo kurudisha fedha hizo.
Katika hukumu hiyo, Hakimu Mazengo
alimwachia huru Maranda baada ya kutoonekana na hatia katika makosa mawili
yaliyokuwa yakimkabili.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo,
Wakili wa serikali, Pius Hilla, aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa
mshtakiwa kwa kuwa makosa aliyoyafanya
yanachangia kuangusha uchumi wa nchi.
Kwa upande wake, Wakili wa utetezi,
Majura Magafu aliiomba mahakama kumpunguzia adhabu mteja wake kwa kuwa anategemewa na familia yake, pia anasumbuliwa
na ugonjwa wa Shinikizo la Damu (BP).
Katika kesi hiyo, Farijala na
Maranda walidaiwa kujihusisha na uwasilishaji wa hati za uongo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zikionyesha kampuni yao ya Kiloloma &
Brothers imepewa idhini na kudai deni la kampuni ya nje ya M/S BC Cars Export
huku wakijua si kweli.
Ilidaiwa kuwa katika udanganyifu
huo, watuhumiwa hao walijipatia sh. milioni 455 kutoka katika Akaunti ya Madeni
ya Nje (EPA).
No comments:
Post a Comment