KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 19 April 2015

WANACHAMA WA CHADEMA KWA PAMOJA WATANGAZA NIA YA UBUNGE NA UDIWANI



Kundi la wanachama wa Chadema, ambao wamejitokeza kwa pamoja kutangaza nia ya kugombea Ubunge na Udiwani katika Jimbo la Segerea jijini Dar es Salaam, leo
CHAMA  cha Demokrasia na Mandeleo (Chadema), Jimbo Segerea jijini Dar es Salaam, kimetangaza  idadi ya watia nia 20 wa Ubunge na Udiwani wa  Jimbo hilo.

Jimbo hilo ambalo lina Kata 13 linaongozwa na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Idadi ya watia nia ya Ubunge wako 20 ambao miongoni mwao wanawake ni wanne, huku wale wa udiwani wako 50 kati ya hao wanawake 10.
  
Akizungumza na waandishi wahabari, leo jijini Dar es Salaam,  alisema watia nia wote wameamua kukutana, kutangaza nia ya Ubunge na Udiwani  kwa pamoja ikiwa ni ishara ya kuweka tofauti zao pembeni.

 “Watia nia wote ni wasomi na wanakubalika nje na ndani ya chama chetu, kauli yetu ni kuruhusu Demokrasia ichukue nafasi kwani tunajua nafasi iliopo ni moja tu, hivyo tutapigania yeyote kati yetu atakayekuwa amepewa ridhaa ya kuwakilisha chama chetu na kwa yule atakayekosa kuteuliwa hatahama kwa sababu ya kutoteuliwa”alisema Kidera.

Kidera, alisema wote wataheshimu maamuzi ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kwa lengo la kumng’oa nduli CCM na vibaraka wake.

Kwa upande wake Stephen Kitomary (Chadema), alisema  amepata msukumo wa kugombea  Ubunge katika jimbo hilo, kutokana na ukwamishwaji wa shughuli za maendeleo na mbunge aliyoko sasa.
“Mbunge aliyekuwepo kwa sasa anaishi eneo la wazi ambalo lilikuwa limetengwa kwa ajili ya kujenga soko, hivyo kusababisha kutokuwepo kwa soko”alisema

Adolfu Mkono, ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM), ametambaye anawania udiwani Kata ya Tabata alidai kuwa anagombea nafasi hiyo kwa ajili ya kupinia haki za wanyonge ambao wametengwa na viongozi walioko madarakani.

 Wakati  wanachama hao wakitangaza nia za kutatua kero za wananchi, mkazi wa Kitongoji cha Kibaoni, Kisarawe  Pwani, Raheli Samweli, amekishukuru Chadema kwa msaada wake wa kumjengea nyumba.

Akizungumza na wandishi wa habari,  Raheli  Samweli, mama wa familia ya watoto  watatu, ambaye kwa sasa ni mjamzito,  alisema mahali anapoishi ni hatarishi, hata hivyo ameomba msaada kwa wadau wengine watakaoguswa wamsaidie.
 
Mwenyekiti wa Baraza  la Vijana  Bavicha  (Bavicha), Kisarawe Baraka Musa (Chadema), alisema kuwa atahakikisha  wanamsaidia mama huyo, ili apate  sehemu nzuri kwa ajli ya malazi.
“Tumejipanga Chadema tutahakikisha  wananchi wote wanaoishi mazingira mabovu tunawasaidia”alisema Baraka.

Musa, alisema kutokana na wananchi wa Kisarawe  kuishi mazingira  hatarishi ameamua kutia nia ya kugombea Udiwani Kata  hiyo,  ambayo kwa  sasa inaongozwa na  Adamu Nimba, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri  Wilaya ya Kisarawe.
Kwa atakayeguswa   wasiliana na  0658 15 24 O9.

No comments:

Post a Comment