KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 19 April 2015

VIONGOZI WA KIROHO, JAMII WAONYWA KUPOKEA FEDHA ZA AIBU



ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi Kaskazini, Fredrick Shoo, amewaonya baadhi ya viongozi wa kiroho na Jamii, kuacha tabia ya kupenda kupokea fedha za aibu ambazo zinawafanya washindwe kusimamia haki za watu wa mungu.

Kauli hiyo aliitoa wakati wa ibada kuwaingiza kazini viongozi wapya watatu na kuwaaga wengine wawili, ibada ambayo ilifanyika katika Usharika wa Azania Front jijini Dar es Salaam jana.

Alizitaja fedha hizo kuwa ni zile zilizopatikana kwa njia ya rushwa, wizi, dawa za kulevya au hata kama ni kwa njia ya sadaka zinazotolewa kwa watumishi wa mungu hizo hazikubaliki kwani matokeo yake ni viongozi hao kupotosha ukweli wa injili.

“Viongozi uwakikosa uaminifu wawe wa kanisa wawe wa kijamii watakosa nguvu ya kukemea rushwa, wizi na mali ya kanisa watakosa nguvu ujasiri wa kukemea wizi wa mali ya umma,”alisema.

Askofu Shoo, alisema vitendo vya matumizi ya fedha ya aibu hayakubaliki kwa yeyote mwenafasi ya kuongoza watu wangu.

Alisema kiongozi bora anapaswa kuwa kielelezo cha kusimamia haki za wale anaowaongoza na si kujifanya kama vile bwana kwa kuwalazimisha watu wamfuate.

Viongozi walioingia kazini

Viongozi walioapishwa jana walikuwa ni Askofu Msaidizi wa Diyosisi ya Mashariki na Pwani, Chadiel Lwiza, Katibu Mkuu Geofrey Mkini na Naibu Katibu Mkuu Boniphace Kombo.

Dk. Alex Malasusa alipokuwa akiwaapisha viongozi hao aliwaasa waende wakatoe huduma hiyo ya kiroho kwa kuzingatia kitabu cha Biblia ambacho ndio muongozo wao.

Walioagwa walikuwa ni Askofu Msaidizi wa Dioyosisi ya Mashariki na Pwani, George Fupe, ambaye alizawadiwa gari aina ya Toyota Double Cabeenna na Katibu Mkuu Balozi Richard Mariki, naye pia alizawadiwa gari aina ya R4.

Akizungumza baada ya kuagwa Askofu Fupe, aliwaasa viongozi wenzake waliyowapisha kwamba waende wakatafanye kazi hiyo ya kuwahudumia wa amini kwa kuzingatia ushirikiano.

“Mwanzo nilikuwa nakutuma sasa umekuwa kiongozi wangu ututume tu na utakapoona tumekosea utusamehe,”alisema Fupe.

No comments:

Post a Comment