JANA jioni, Tanzania
Daima liliwasiliana kwa njia ya simu na Msemaji wa Umoja wa Madereva
Tanzania, Rashid Saleh kutaka kujua walichokubaliana na alisema: “Tumeyamaliza
na serikali imetupa siku 30 kuanzia leo (jana) yataisha.” Hivyo Juni 4 mwaka
huu itakuwa mwisho wa siku 30.
Alisema baadhi ya mambo yatakayoshughulikiwa ndani
ya kipindi hicho ni pamoja na mishahara na posho, bima ya afya, suala la
kutokurudi darasani kusoma nalo limefutwa sanjari na mikataba yao kuandaliwa
yenye ubora na si bora mikataba.
Salehe alisema mazungumzo yalikuwa mazuri na kwamba
wamefurahi kwani katika kamati iliyoundwa ya watu 15 walipewa nafasi tano za
uwakilishi. “Tutachaguana madereva wa bodaboda, malori, mabasi na wengine
tutakaoona wanafaa,” alisema.
Alitaja viongozi waliohusika katika majadiliano
hayo kuwa ni; Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, Waziri wa Viwanda na Biashara,
Dk. Abdallah Kigoda, Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga, Waziri
wa Fedha, Saada Mkuya, Msaidizi wa Waziri Mkuu (hakumtaja jina lake), Waziri wa
Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda na
viongozi wa madereva. Kikao hicho kilifanyikia Ofisi ya Waziri Mkuu.
“Nimemaliza kuwatangazia wenzangu hapa sasa hivi
(Ubungo) na kazi zinaendelea kama kawaida na tunachokisubiri sasa ni
utekelezaji tu,” alisema.
CHANZO TANZANIA DAIMA
No comments:
Post a Comment