KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday 16 July 2015

HIVI NI KWELI ENEO LA JANGWANI WAMEPEWA WAMACHINGA AU NI KIINI MACHO?

MAKALA

HALI ya sintofahamu kuhusu kupewa eneo la kufanyia biashara kwa wafanyabiashara ndogo ndogo (Wamachinga), kuna madai kuwa ugawaji wa eneo hilo la Jangwani, hauzingatii utaratibu wa kujali haki za walemavu.
Hivi karibuni wafanyabiashara wa maduka makubwa walikwenda kumlalamikia Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, kwamba wamachinga walikuwa wakivuruga biashara zao, kwa kupanga bidhaa zao nje ya maduka yao.
Baada ya malalamiko hayo, Mkrugenzi huyo aliitisha kikao kwa ajili ya kutafuta muafaka wa mvutano huo, hata huvyo mwisho wa siku ikatokea wamachinga hao kutakiwa kuhamia Jangwani.
Kwa ujumla baada ya wamachinga hao ambao wamechanganyika na watu wenye ulemavu, kupata taarifa hizo, wale wenye viungo kamili walikwenda kuvamia maeneo ambayo wanaona yanafaa.
Kuvamia huko kulitokana na kutokuwepo utaratibu wowote uliyokuwa umepangwa na viongozi wa manispaa hiyo.
Utaratibu huo mbovu ulisababisha watu wenye ulemavu washindwe kupata maeneo hayo ambayo pia yameingiliwa na matapeli.
Matapeli hao baada ya kusikia kuwa wafanyabiashara wameruhusiwa kufungua bishara zao, walifika mapema na kushika maeneo ambayo hivi sasa wanayauza kati ya sh. 180,000 hadi sh. 300,000.
Hali hiyo imewafanya watu wenye ulemavu kuendelea kuteseka kutokana na kushindwa kupata fedha, hizo ambazo wakizitowa watakuwa wameua msingi wa biashara zao.
Matapeli hao bila aibu wamejivika uhalisia wa kuwa wamiliki wa maeneo,wakidai ni ya kwao hivyo kila anayetaka lazima awaone wao bila hivyo hakuna atakayepa.
Labda, ni kichangia klatika hili naweza kusema kwanza uongozi wa manispaa ya Ilala imekosea kwani haikuweka utaratibu mzuri akatika ugawaji wa maeneo hayo.
Baadhi ya wandishi siku wamachinga hao wanakwenda katika eneo hilo bahati mbaya hakukuwa na kiongozi wa aina yeyote ambaye angeweza kutoa malekezo.
Hali hiyo ndio imesababisha vurugu zote hizo kwa mtu mmoja kumiliki maeneo makubwa na kuanza kuwauzia wengine kinyume cha sheria.
Kinachoshangaza hadi naadika makala haya hakuna  kiongozi hata mmoja aliyefika kujionea maendeleo ya wafanyabiashara hao.
Pamoja na nia njema ya serikali ya kuwasidia wafanyabiashara, ili wafanye biashara zao kwa amani lakini bado kuna maswali mengi kuhusu eneo hilo.
Maswali hayo yanatokana na ukweli kwamba eneo hilo bado halina huduma za kijamii kama vile vyoo na mabomba ya maji jambo linalowashangaza wananchi.
Inaonekana uongozi wa wilaya hiyo umekurupuka kwani haikuwa na mpango wa kuwapeleka pale isitoshe haieleweki eneo hilo litakuwa la kudumu kwa wafanyabiashara hao au la.
Maswali hayo yanatokana na ukweli kwamba eneo hilo waliwahi kupewa madereva wa Fuso kama eneo lao la kuegeshea magari baada yakutotakiwa kuonekana katikati ya jiji.
Madereva hao walipwa eneo hilo kwa sherehe kubwa na aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa huo, Yusufu Makamba, tena wakati huo pakiwa pamejengwa miundombinu muhimu.
Makamba, aliwajengea vyoo, mabomba ya maji na kituo cha Polisi, hata hivyo katika mazingira tata madereva hao walikuja ondolewa na Mkurugezi wa jiji, bakari Kingobi kwa madai kuwa madai kuwa walipelekwa kimakosa na kwamba alikuwa hawatambui kwa vile hawakuwa na nyaraka zinazothibitisha uwepo wao.
Nimekumbushia hilo, nikiwa na maana kwamba utaratibu uliotumika unatiashaka kwamba huenda kupelekwa pale ikawa ni mtego ili baadae waje kuwaondoa tena kwa visingizio vyovyote wakati huo.
Ili kuepuka mgogoro mwingine ni vema uongozi ukajitokeza kuwahakikishia wafanyabiashara hao kwamba haita waondoa kama walivyowaondoa madereva wa maroli.
Uongozi huo uwaeleze kuwa eneo lile hivi sasa linatumika kinyume na awali kwamba lilikuwa eneo la bondeni na hatarishi kwa sababu za kuitwa hivyo bado zipo na kubwa zaidi ni mvua.

Ushauri wangu kwa machinga ni kwamba wasiwekeze nguvu zao zote kwa kuamini kwamba huenda wakaishi hapo milele wanaweza kuja kujuta kwani serikali hii ni kigeugeu, ambayo haijali matatizo ya wananchi wake.

No comments:

Post a Comment