KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday 8 July 2015

JANUARY AHUZUNISHWA, MAISHA YA ALBINISM BUHANGIJA


MAKALA
WAZAZI wenye watoto katika kituoni cha kulelea watoto wenyemahitaji maalum Buhangija mkoani Shinyanga wamewatelekeza watoto hao kwa zaidi ya miaka sabab sasa.
Watoto hao ni wale wenye ulemavu wa ngozi (Ualbino), ambao wamewapeleka kituoni hapo kwasababu huko vijijini watoto hao wanawindwa na wauwaji  kutokana na imani za kishirikina.
Kutokana matukio ya kuwindwa watoto hao na wao kuogopa kufanyiwa vitendo vya kikatili hivi sasa kituo hicho kimekuwa kikipokea watoto watatu hadi watano kila siku kutoka maeneo mbalimbali ya mikoa ya kanda ya Ziwa.
Kutokana na ongezeko hilo, kituo hicho kinakabiliwa na matatizo mengi ikiwemo kukosefu wa huduma za kijamii huku baadhi ya wazazi wa toto hao hawajulikani waliko kwani hata anuani walozoacha awali hazipatikani na hata maeneo waliyokuwa wakiishi wamehama bila ya taarifa.   
Kituo hicho awali kilikuwa kikipokea fedha kutoka serikalini ambapo bajeti inayotengwa ni kwa ajili ya watoto 50, hata hivyo fedha hizo kwa sasa hazitoshi kutokana na wingi wa watoto kituoni hapo.
Hivi karibuni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknoloji, January Makamba, akiwa  Shinyanga kutafuta wadhamini, wananchi waeneo hilo walimuomba ende kituoni hap kwa ajili ya kujionea maisha ya watoto hao.
Makamba alifanya mazungumzo na wadau kadhaa wa harakati za kupinga mauaji ya albino, ndipo akatajiwa kituo hicho.
Baada ya kutajiwa kituo hicho alikubali kutembelea kituo hicho baada ya shughuli ya kupata udhamini kukamilika, kwamba angetumia walau hata nusu saa katika kituo hicho cha Buhangija.
Kutokana na hali ya kukatisha tamaa aliyoikuta kituoni hapo Makamba na msafara wake wakiwemo wandishi wa habari walikaa saa tatu.
Yote hayo yalitokana nakuguswa na mazingira na changamoto za kituo kile, zaidi na upendo wa watoto wale kwa kuwa saa zote walipenda kubebwa na kushikwa na kukumbatiwa.
Kwa asiyejua hali ya maisha ya watoto hao katika kituo hicho, basi ni vema mkatambua kuwa kinahitaji msaada mkubwa.
Katika kituo kile kuna shida ya kila kitu ikiwemo mabweni, vitanda, magodoro, shuka, vyandarua, mashuka, madawa - kila kitu, lakini shida kubwa zaidi ni vyakula.
Kwa siku kituo hicho kinatumia kilo 70 za unga/mchele, kilo 70 za maharage, bado mafuta, sukari na maji ambako Mkaa unaotumika kwa siku ni gunia moja na nusu. Makamba katika kutembelea kituo hicho kuwa watoto hao wana ndoto kubwa za maisha yao ya baadae, lakini pia wanajua kwamba maisha yao yako hatarini na wale wadogo zaidi wanapata shaida kuelewa ni kwa nini.
 Baada ya kuzungumza na walimu kuhusu kuwa na utaratibu endelefu wa kupata rasilimali za kuendesha kituo hicho, na kwamba kuna mawazo kadhaa ya kufanyiwa kazi.
Aidha, kutokana na matatizo hayo makubwa yaliyoko kituoni hapo bado misaada inahitajika hivyo basi kama yupo atakayeguswa wasiliane na Mwalimu Peter Ajari kwa namba ya simu 0757 611 930.
 Nikiwa mmoja wa wandishi waliofika kitoni hapo niseme tu kwamba hali katika kituo hicho ambacho kina watoto zaidi ya 300 hali ni mbaya hivyo ni wakati kwa jamii kuwakumbuka watoto hao.
Mtoto mdogo kuliko wote katika kituo hicho ana miezi 18 na mkubwa zaidi ana miaka 24, ukiongea nao, wana ndoto kubwa za maisha yao.
Hata hivyo kuna haja ya kuwapongeza baadhi ya wafadhili na taasisi ambazo zimekuwa zikisaidia kituo hicho kwa mfano kuna taasisi zimeajiri walimu na walezi wa ziada.
Mwisho ni ungane na kauli ya Makamba kwamba hata kama huna cha kutoa basi ukifika Shinyanga, usiache kutembelea Buhangija kwasababu watoto hawa wanahitaji pia upendo, kwani wengi wao wazazi wao walivyowaacha hawajarudi tena.
Makamba, katika ziara yake hiyo, alitoa msaada wa unga wa sembe kilo 500, maharage kilo 500, mchele kilo 500, mafuta ya kula, sabuni na vitu vingine.
Pamoja na yote hayo, nawasihi wazazi waliowatekelekeza watoto kubadili msimamo huo, na baadala yake wajitokeze katika kutoa ushirikiano wa kimalezi kitendo ambacho kitawaletea faraja watoto hao.

No comments:

Post a Comment