KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Thursday 9 July 2015

MO AWAAGA WAKAZI WA SUNGIDA

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayemaliza muda wake, Mohammed Dewji (Mo) ametangaza  kustaafu rasmi siasa na kutogombea tena ubunge baada ya kuliongoza jimbo hilo kwa miaka 10.
Dewji alitangaza uamuzi huo jana,  katika Viwanja vya Peoples Club mjini hapa huku akishuhudiwa na umati mkubwa wa watu  waliofurika kutoka kila pembe ya  Singida mjini.
Alisema amechukua  uamuzi huo  baada ya kulitumikia jimbo hilo  kwa muongo mmoja  hivyo ameamua kutoa fursa kwa makada wengine wa chama hicho kuendeleza mazuri aliyoyafanya katika kipindi cha ubunge wake.
Alibainisha kuwa kutokana na kubanwa na majukumu mengine ameamua  kwa ridhaa yake mwenyewe pasipo kushinikizwa na mtu yeyote kuachia jimbo.
 “Nimeamua kwa ridhaa yangu kutangaza kutogombea tena ubunge katika jimbo hili ili kutoa nafasi kwa makada wengine wa CCM  Singida Mjini  kuwania nafasi hiyo,” alisema.
 Alisema alipoanza safari yake ya siasa, lengo kuu lilikuwa  kuleta matumaini kwa watu wa Singida  mjini  kwa sababu  palipo na matumaini kila kitu kinawezekana hivyo  uamuzi wa kutogombea unabaki palepale .

Mafanikio

Akizungumzia mafanikio, alisema katika ubunge wake alijenga shule 15 za sekondari za kata  kutoka mbili alizozozikuta mwaka 2005. Pia alisaidia watoto 15,000 ambao wazazi wao hawana uwezo katika masomo yao na kujenga Zahanati za Mungumaji na  Manga ambazo zimekamilika na katika Kijiji cha Ititi bado ujenzi unaendelea.

 Alisema alijenga vyumba vya madarasa pamoja na kusambaza madawati katika shule zote za msingi katika jimbo lake. Pia alitoa vyandarua zaidi ya 6,000 kwa ajili ya kinamama na watoto jambo ambalo limeonyesha mafanikio kwa asilimia 50, na kupeleka madaktari  bingwa ambao waliweza kufanya upasuaji kwa watu 1,000 waliougua mtoto wa jicho.

No comments:

Post a Comment