Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, (SACP), Simon Siro. |
BAADHI ya wakzi wa jiji la
Dar es Salaam wameitaka serikali kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa zinazotolewa mara
kwa mara n vyombo vya habari kwamba nchi hivi sasa inakabiliwa na tatizo la
ugaidi.
Wakazi hao walisema hivyo
baada ya hivi karibuni kusambaa kwa tarifa kuwa mkoani Morogoro kulitokea
mapambano kati ya magaidi 50 na polisi.
Walisema wanaitaka serikali
kupitia Jeshi la Polisi kufanya hivyo kwa vile wananchi hivi sasa wanaishi
wakiwa na wasiwasi huku baadhi yao wamelazimika kuyama makazi yao kutokan na
hofu ya kushambuliwa.
Hamisi Dihule, mkazi wa
Mansese ambaye asili yake ni mkoani Morogoro, alisema ukimya wa serikali katika
kulitolea ufafanuzi suala hilo kunawafanya wananchi washindwe kuelewa kuhusu
ukweli taarifa hizo zinazozagaaa kila kukicha.
Alisema, ktika kuendeleza
hofu kwa wananchi, juzi kuna taarifa kutoka mkoa wa Pwani ambazo
zilithibitishwa na Kamanda wa Mkoa wa Pwani kwamba kuna kikundi cha magaidi
kilitelekeza silaha baada ya mapambano na polisi.
Silaha zilizotelekezwa
zilikuwa ni risasi 50 za shotgun, bomu moja lililotengenezwa kienyeji fulana
tatu, kitabu kimoja cha kuruani, jambia moja na begi moja.
“Hiki kitu si cha
kushabikia kwa sababu hata kuwatajataja magaini ni hatari na zaidi wapo
wanaosema magaidi hao ni El Shabab,”alisema Dihule.
Dihule, alisema kitendo cha
kukitaja kikundi hicho ambacho hakina mpango wa kushambulia nchi hii, kinaweza
kuwajengea hasira na kikaamua kutekeleza mashambulizi kweli.
Sharifa Hamisi, alisema
haamini kama watu hao wanaokamatwa kama kweli ni magaidi, bali anawachukulia
watu hao kama wahalifu na vibaka tu.
Alisema hivyo, haingii akiakili
kuwafanya watu hao waliokamatwa ktika maeneo ya mashamba huko wakafananishwa na
magaidi, akibainisha kuwa wakati umefika kwa polisi kutoa taarifa kuhusu
taarifa hizo na ikiwezkana kuwataka wanaotoa taarifa hizo kuacha kufanya hivyo.
No comments:
Post a Comment