KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday 7 July 2015

SEMTAWA: CKUT WAZALENDO KITASHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2015

Mwenyekiti na Muasisi wa Chama cha Kijamaa na Uzalendo Tanzania (CKUT), Ramadhani Semtawa, akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, Noel Antapa
MWENYEKIT wa Chama cha Kijamaa na Uzalendo Tanzania (CKUT), Ramadhani Semtawa, amesema chama hicho kitarajia kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Chama hicho kilipta usjili wa muda tangu Aprili 13 mwaka na kilpaswa kupata usajili wa kudumu ndani ya miezi sita, baada ya kupata wanachama katika mikoa kumi nchini.
Semtawa, aliyasema hayo wakati alipozungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kuhusu kama chama hicho kitashiriki uchaguzi huo au la.
Alisema hivyo kwa vile hadi sasa chama hicho kimemaliza kazi ya kupata wanachama katika mikoa kumi nchini, kati ya hiyo miwili ikiwa ni kutoka Zanzibara, tayari wamekwisha kabidhi makablasha ya wanachama hao kwa Msajili wa Vyama tangu Julai 1 mwaka huu.
Aliitaja majina ya mikoa walikokwenda kupata wadhamii hao kuwa ni pamoja na Dar es Salaam, Pwani, Tana, Tabora, Lindi, Mtwara, Dodoma, Morogoro kwa upande wa Bara na Kusini Pemba na Mjini Magharibi Tanzania Zanzibar.  
Semtawa, alisema baada ya hatua hiyo wanamsubiri utaratibu wa Msjili wa kuhahakiki, baada ya kuwaona wanachama hao, atato cheti cha usajili wa kudumu, ambacho kitawafanya washiriki uchaguzi huo.
“Kimsingi chama hicho kinaimani kubwa na Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa chini ya Jaji Francis Mutungi na wasaidizi wake  Sisty Nyahoza, hivyo tunaimani uhakiki utakwenda vizuri tu.
“Baada ya hapo tutakuwa tumekamilika kichama, tutaweza kusimamisha wagombea katika majimbo na Kata lakini  kwa sasa tuna uhuru wa kupeperusha bendera, kufungua matawi na kufanya mikutano ya hadhara,”alisema Semtawa.
Semtawa, lisema shabaha yao kubwa katika uchaguzi huo ni kusimamisha wagombea katika udiwani na umbunge kwa lengo la kuzishika Halmashauri.
“Sisi tuko tayari bali tunamsubiri Msjili wa Vyama atuite wakati wowote kuanzia hata kesho kwa ajili ya kuhakiki majina hayo kwani akifanikiwa katika kipindi hiki cha Julai mwaka huu, tutaweza kwenda sambamba na ratiba ya uchaguzi huo,”alisema Semtawa.
Alisema, Ratiba ya uchaguzi huo inaonesha kuwa Agosti 22 mwaka huu ndio siku ya kuanza kampeni.


No comments:

Post a Comment