KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Sunday 2 August 2015

DK. MILTON MAKONGORO MAHANGA HUYOO CHADEMA KAMA LOWASSA

Dk. Mahanga, akionesha kura feki, wakati alipozungumza na wandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Milton Makongoro Mahanga, ametangaza kujivua uanchama wa chama hicho, anakusudia kujiunga na Chama cha Demeokrasia na Maendeleo (Chadema).
Dk. Mahanga, alisema amefikia uwamuzi huo baada ya baadhi ya vigogo kuanzisha operesheni ya kumuondoa katika ubunge Jimbo la Segerea.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Dk. Mahanga, alisema katika ushindani wowote kuna kushinda na kushiwandwa, kama angeshindwa kwa halali wala asingekuwa na kinyongo chochote.
Alisema amefikia hatua hiyo kutokana na mfumo mbovu wa CCM unaowapa viongozi wachache uhalali na kiburi cha kufinyanga demokrasia na kuendeleza dhuluma.
Dk. Mahanga, alisema mfumo pamoja na hila umekuwa ukiwanyima haki baadhi ya wagombea  bora hivyo kukiangamiza taratibu chama hicho.
“Niweke wazi kwamba sina ugomvi hata kidogo na wanachama walio wengi wa CCM katika jimbo la Segerea amabao kwa miaka 15 wamenipa ushirikiano mzuri sana katika kuleta maendeleo katika jimbo hili la Segerea ikiwemo barabara,”alisema.
Aidha, alisema  katika kura za maoni za kuwapata wagombea wa udiwani na ubunge katika jimbo hilo, kulikuwa na upendeleo wa wazi  hususan kwa Bonna Kalua.
Dk. Mahanga, alisema mazingira na ushahidi mbalimbali ulonesha ni jinsi gani Bonna alivyobebwa na wizi wa kura uliofanywa na mgombea huyo na washirika wake hadi kuugeza uchaguzi huo kuwa kituko mbele ya wanachama wengi wa CCM.
Alisema licha ya malalamiko mengi aliyotoa kwa mdomo, simu na barua, uongozi wa CCM wilaya, Mkoa na Taifa haukuchukua hatua zozote za maana na yaonekana wazi uongozi huo ulikuwa sehemu ya mpango mzima wa kuhakikisha anashindwa katika uchaguzi huo. x “Rejea barua zangu kwa Katibu wa wilaya na Katibu Mkuu, kama vile barua Kumb. SEG/CCM/02/14 ya tarehe 28/72014; SEGCCM/03/14 ya tarehe 04/08/2014; SEGCCM/04/14 ya tarehe 19/8/2014; SEGCCM/05/14 ya tarehe 19/8/2014 na SEGCCM/01/15 ya 21/01/2015,”alisema Dk. Mahanga.
 Akizungumzia mpango wa operesheni ya ‘Ondoa’ Mahanga, alisema ilianza muda mrefu, lakini ilishika kasi wakati na baada ya vikao vya CCM Taifa vya kusaka mgombea urais mjini Dodoma mwezi uliyopita.

Dk. Mahanga, alisema kule Dododma kuna familia ya kigogo mkubwa wa CCM Taifa ambaye hakuweza kumtaja jina, iliyokuwa ikiishi jirani na nyumbani kwake iliamua hata kuisakama familia yake.
Alisema familia hiyo ya kigogo ilifikia kuwaeleza wanaye kwamba baada ya kuondoka Waziri Mkuu wa zamani Eduard Lowssa sasa itakuwa ni zamu ya baba yao kuondoka Segerea kwa gharama yeyote.
Dk. Mahanga, alisema baada ya kauli hizo ndipo fedha nyingi ziliingizwa jimboni  kwake na kufikia mikononi mwa Bonnah amabye alianza kuzigawa kwa wingi na jeuri kupindukia.
Alisema baada kuingizwa fedha hizo, ghafla walikuja wagombea wengine wapya ambao wengine walijidai kwamba wametumwa kwa kazi maalum ya kumzuia Dk. Mahanga kushinda ubungea kwa kugawa zile kura.
Dk. Mahanga alisema kuwa kura amabzao zilionekana wazi zingekuwa za kwake ili kumpa Bonnah nafasi kubwa ya jushinda kura hizo za maoni.

Aliongeza kwa kusema kuwa licha njama zote alizozitaja hapo juu kuumbeba Bonna, bado njama zilifanyika za kumpa kura za wizi, na makaratasi mengi ya kura yaliyotolewa kwenye maeneo ambapo yalikuwa tayari yamewekewa alama ya vema kwenye jina la Bonnah.
 Dk. Mahanga alisema baada ya utaratibu huo kazi ikawa ni ya kuzitumbukiza kura hizo kwenye masanduku ya kura.
 Hata hivyo, baadhi ya wanachama wema waliweza kugundua njama hizo na kufanikiwa kukamata vitabu vya makaratasi ya kura yakiwa yameshawekewa alama ya vema kwenye jina la Bonnah.
“Mfano ni kitabu cha karatasi za kura Na. 4401-4500 na 27801-27900 ambavyo ni sawa na kura 200 zilizokamatwa maeneo ya Kata ya Kinyerezi. “Yaonekana maelfu ya karatasi kama hizi zilitumika maeneo mengi ya jimbo kumpa ushindi wa bamdia Bonnah,”alisema Dk. Mahanga.
Alisema fedha katika kura hizo ziligawanywa katika jimbo hilo hadi siku ya kupiga kura, baadhi ya maeneo wanachama walipewa sh. 10,000 kila mmoja huku wengine wakipewa kadi mpya hususan vijana wakipewa kadi mpya zenye majina feki.
 Dk. Mahanga, alisema alishindwa kukata rufaa kutoka na mfumo mzima kuonekana kupuuza malalamiko yake kwani tayari alikwishaandika barua zaidi ya kumi hivyo madai yake yasingeweza kusikilizwa.

MJUWE DK. MAHANGA

Dk. Milton Makongoro Mahanga
amezaliwa katika kijiji cha Mugeta wilaya ya Mara Kusini (sasa Bunda) Aprili 3, 1955. Akina mama wawili wa kabila la Waikizu waliomsaidia mama yake kujifungua, waliwaomba wazazi wake wakubali kunipa jina la Makongoro ambaye alikuwa Chifu wa Waikizu ingawa asili yake ilikuwa ni wilaya ya Mara Kaskazini (sasa Rorya).

Wazazi wake walikubali na mpaka sasa anatumia jina hilo la Makongoro. 
Baadaye walihamia wilaya ya sasa ya Serengeti ambako alisoma katika Shule za Msingi za Kyambai (sasa Matare) na Mugumu katika wilaya hiyo ya Serengeti na Bukama Ikizu katika wilaya ya Bunda kati ya mwaka 1965 na 1971. 
Mwaka 1972 hadi 1975 alisoma kidato cha Kwanza hadi cha Nnne katika Shule ya Sekondari Mara na baadaye kumaliza masomo ya Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari Tambaza jijini Dar es Salaam.
Kuanzia mwaka 1978 hadi 1980 alichukua masomo ya Shahada ya Kodi na Uhasibu katika Chuo cha Fedha (IFM), jijini Dar es Salaam. Kupitia Bodi ya Ununuzi na Ugavi ya NBMM (sasa PSPTB) nilikuwa Mtanzania wa kwanza kupata Stashahada ya Juu ya Ununuzi na Ugavi CSP (sasa CPSP) inayotolewa na NBMM mwezi Mei 1980. 
Aidha kwa mara nyingine alikuwa Mtanzania wa Kwanza kuwa na CSP na CPA kwa pamoja pale alipofanikiwa kupata Stashahada ya CPA inayotolewa na Bodi ya Uhasibu (NBAA) mwezi Mei 1983. Baadaye, akiwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) niliamua kusoma na kutunukiwa cheti cha uzamili kwenye masuala ya fedha (MSc Finance) mwaka 1997 kupitia Chuo Kikuu cha Strathclyde cha Glasgow nchini Uingereza.
Kupitia utafiti wa kina nilioufanya nchini Tanzania na nchi nyingine kama Uingereza, Kenya na Uganda kuhusu mahusiano kati ya umasikini na makazi duni mijini, nilifanikiwa kutunukiwa Shahada ya uzamivu (PhD) kupitia Chuo cha Washington International University cha nchini Marekani Julai mwaka 2000. Kwa umahiri wake, utafiti wangu huo uliweza kuchapishwa mwaka 2002 na wachapishaji wa Dar es Salaam University Press (DUP) kama kitabu: “Urban Housing and Poverty Alleviation in Tanzania” kwa namba ISBN 9976-60-343-6.
























No comments:

Post a Comment