KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Monday 15 February 2016

JAFO AAGIZA IKIFIKA MACHI 15 MAJIKO FERI YAFANYE KAZI



UMOJA wa Wakaanga Samaki katika Soko la Feri Dar es Salaam (Uwasaso), wamepatiwa majiko 48 ya gesi ambayo yatawasaidia kuondokana na utumiaji wa majiko ya kuni ambayo hutoa moshi mwingi, hatari kwa afya zao.
Kwa muda mrefu Wakaanga samaki hao wamekuwa wakifanyakazi katika mazingira magumu kutokana na matumizi ya majiko ya kuni ambayo yamekuwa yakichangia uchafuzi wa mazingira katika eneo hilo ikiwemo Ikuku.
Akizungumza namwandishi wakati akiwa katika shuguli zake za uzalishaji jijini leo, Mwenyekiti wa Uwasaso, Cyril Nyange, alisema majiko hayo yametengenezwa na Kampuni ya Envotech Tanzania Limited ambayo wameyakubali kutokana na ubora wake ukilinganisha na ya awali yaliyokuwa yakitumia mkaa.
Alisema, majiko hayo yanatarajiwa juanza kutumika Machi 15 mwaka huu, baada ya kukamilika uezekaji wa paa la jengo la jiko hilo la samaki kama ilivyoagizwa, Naibu Waziri wa Tamisemi Seleman Jafo.
Alisema, kutokana na ubora wa majiko hayo, wanatarajia kuwa yatasaidia kuboresha uzalishaji zaidi huku yakiimarisha usafi wa mazingira, hali ya afya zao na kuongeza wateja ukilinganisha na sasa.
“Waziri alikuja hapa na kuwaagiza uongozi wa Manispaa ya Ilala kuwa inahakikisha majiko hayo ikifika tarehe hiyo lazima yaanze kazi huku akiwahakikishi kuwa atakuwepo katika soko hilo siku hiyo.
“Pamoja na kuwa karibu Ikulu, tumekuwa tukitumia kuni ambazo moshi wake mbali na kuathiri afya zetu lakini pia ulikuwa ukiingia Ikulu.
“Yatakapoanza kazi watu wataupenda kwani tutakuwa tunavaa suti kama vile tuko katika ofisi kubwa hakutakuwa na moshi labda mvuke kidogo wa mafuta,”alisema Nyange.
Nyange, alisema hivi sasa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo ya Ilala, Issaya Mngurumi, yuko katika mazungumzo na kampuni za usambazaji wa gesi ili kupata gesi ya kuanzia katika majiko hayo.
Jiko hilo lina umuhimu mkubwa kwa vile linahudumia karibu mikoa yote iliyoko nchini, hivyo kuimarika kwake kutapunguza kero ya foleni wateja wanaofika kwa ajili ya uzalishaji wa wasamaki wanapotoka baharini.

No comments:

Post a Comment