WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, amesema kampeni ya serikali ya
awamu ya tano katika kupambana na baadhi ya watu wanaopenda kufanya kazi kinyume cha sheria za
nchi haina nia ya kumuoenea mtu.
Majaliwa, alisema mara baada ya kuanza kampemi hiyo
inayoambatana na kaulimbiu ya Hapa Kazi Tu, kumezuka manung’uniko kwa baadhi ya
watu kutokana na hatua hizo zinazo chukuliwa na serikali katika kuwaajibisha
watendaji wa umma na baadhi ya wafanyabiashara.
Hayo aliyasema jijini Dar es Salaam jana, wakati wa Mkutano
wa Wadau, wa kutoa taarifa ya hali ya kiuchumi na maendeleo ya Mkoa wa Rukwa na
Katavi.
Majaliwa, alisema lengo la kampeni na kaulimbiu hiyo ya
hapa kazi tu inalenga kuwakumbusha wananchi wote kuwajibika kwa bidii katika
kila sekta husika ili kila mmoja azalishe vya kutosha ili kutunisha pato la
taifa.
“Wote mnatambua kwamba ili kutimiza ahadi hizi ambazo
viongozi wa serikali hii ya awamu ya tano tumezitoa ni lazima tuwe na rasimali
fedha za kutosha, napenda kusisitiza umuhimu wa kila mmoja kutimiza wajibu na
jukumu la kuchangia ili kupata fedha za kutosha kutuwezesha kutekeleza yale
tuliyojipangia,”alisema Majaliwa.
Katika kusisitiza hilo, Majaliwa alisema kama ni
mfanyabiashara lazima afanye biashara halali na kuhakikisha kuwa analipa kodi halali
kwa serikali yake, kwamba serikali haitamvumilia mtu atakayejaribu kuzorotesha
juhudi zinazofanywa na serikali katika upotevu wa mapato.
“Kama wewe ni mkulima lazima ulime kwa bidiii, uzalishe vya
kutosha na mazao hayo yapate masoko, yauzwe na fedha zipatikane tulipe kodi ili
kutuwezesha kutekeleza miradi hiyo.
“Kama ni mwana viwanda lazima kuzalisha bidhaa zenye ubora
na bei yake iwe yakuridhisha kwa mtumiaji wa bidhaa hizo, lazima mwenye viwanda
kulipa kodi halali kwa serikali kulingana na taratibu za kodi.
“Na kama wewe ni mtoa huduma za jamii iwe ni katika sekta
ya Elimu, Afya, Maji na nyingine ni lazima kuhakikisha kwamba mnatoa huduma kwa
kuzingatia maadili, kanuni na taratibu za kazi yako,”alisema Majaliwa.
Maliwa alitoa wito kwa Watanzania wote kwa kuwataka
kumsaidia Rais John Magufuli ili aweze kutimiza la Kaulimbiu ya Hapa Kazi Tu
kwa weledi na maadili katika sehemu za kazi.
Akizungumzia kuhusu Kongamano hilo, Waziri Mkuu, alisema
itaunga mkono kila azimio litakalopitishwa kwa ajili ya masilahi ya wananchi wa
mikoa hiyo tena bila ya kuwaangusha kama ilivyowaahidi katika mikutano ya
kampeni.
Aidha, alisema pamoja na fursa walizonazo bado kuna
matatizo yanayohitaji kufanyiwa kazi kwani mikoa hiyo kwa muda mrefu haijawahi
kuwa mikoa yenye ukame wa kutisha.
Alisema hiyo ndiyo sababu wafugaji wengi wametambua hilo na
sasa wanaikimbilia mikoa hiyo.
“Tahadhali iliyoko ni kujiridhisha kama mifugo inayoingia
kwa wingi kutoka mikoa na maeneo mengine inadhibitiwa, lazima kujiridhisha
kwanza kama kasi ya mifugo inayoingia inaendana na maeneo yaliyotengwa rasni
kwa ajili ya mifugo nay ale ya kilimo.
Tuchukue tahadhari mapema ya kutoanzisha migogoro ya
wakulima na wafugaji katika mikoa hii,”alisema Majaliwa.
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Ibrahim Msengi na mwenzake
wa Rukwa kwa nyakati tofauti, walisema pamoja na mipango ya serikali bado
Jumuiya ya Wanarukwa na Katavi wanaona vipaumbele, vikuu kwa maendeleo ya
wananchi ambayo vinapaswa kusukumwa kwa kasi ya kutosha ni; Miundombinu ya
barabara, maji, umeme, elimu, afya na uchumi.
MWISHO
No comments:
Post a Comment