KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Wednesday 27 April 2016

MAGENGE YA PANYA ROAD YAUWA KIBAMBA NA MSAKUZI



KAMANDA WA KANDA MAALUM, SIMON SIRRO

MAGENGE ya uhalifu maarufu kama ‘Panya Road’ yameendelea kuvamia mitaa, safari hii ikiwa Manzese- Kibamba na Msakuzi- Mbezi wilayani Kinondoni jinini Dar es Salaam, ambapo ndani ya wiki moja iliyopita yameua watu wawili na kujeruhi kwa kutumia silaha za moto.
Hata hivyo, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni amesema kama magenge hayo yamefikia hatua ya kutumia silaha za moto basi yatakuwa ni majambazi hivyo ameyataka yakatafute kazi nyingine halali kwani hata kubali kuona yanaendelea kunyanyasa wananchi.
Magenge hayo hujulikana  kwa majina tofauti katika mtaa husika, mfano mbwa mwitu, machizi 70, watoto wa mbwa, Hapa Kazi Tu, na wadudu wa dampo.
Ndugu wa marehemu hao kwa nyakati tofauti walisema magenge hayo hivi sasa yanafanya unyama huo kwa kujiambini kana kwamba hakuna vyombo vya usalama.
Akizungumzia tukio la mauaji ya Msakuzi Mbezi jana, ambalo limetokea juzi Aprili 23 mwaka huu, mmoja wa mashuhuda, Amiri Masagati, alisema Msonje Mnyampala (22),  aliuawa baada ya kupigwa risasi mgongoni wakati akikimbia genge hilo la wahalifu.
“Hiki kikundi kilituvamia muda wa saa 2:00 usiku kikiwa na gari ambayo hakiujua ila ilikuwa Pickup, wakati tukiwa kijiweni tukinywa kawa ndipo walipotuambia tulalale chini na kutuamlisha tutoe simu zetu na fedha lakini wakati wanafika marehemu alikuwa amekwenda kujisaidia haja ndigo.
Mara baada ya kurudi na kuona tumelala chini ndipo alipouliza kuna nini akajibiwa na wahalifu hao kwa kumtaka alale chini hata hivyo akadhani ni utani lakini akabaini hali siyo shwari ndipo alipojaribu kukimbia,”alisema Masagati.
Alisema baada ya kukimbia mmoja wa wahalifu hao alifyatua risasi hewa kama ishara ya kumtaka kujisalimisha hata hivyo alizidi kukimbia ndipo alipopigwa risasi ya mgongoni na kufariki papo hapo.
Aidha, Masagati alisema baada ya tukio hiyo, siku iliyofuata Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo, ambaye hakumtaja jina pamoja na Mbunge wa Kibamba (Chadema), John Mnyika walifika kutoa pole kwa wafiwa.
Mwili wa marehemu umesafirishwa juzi kuelekea nyumbani kwao mkoani Dodoma kwa ajili ya mazishi.
Naye shuhuda wa tukio la Manzese Kibamba, ambaye hakupenda kuandikwa jina lake gazetini, alisema tukio hilo la mauaji limetokea Aprili 17 mwaka huu baada ya kundi hilo lililokuwa na silaha za jadi na za motokuvamia nyumba zaidi ya tano na kupora mali mbalimbali ikiwamo fedha.
Alisema, aliyeuawa katika tukio hilo alikwa ni jirani yake aliyetambulika kwa jina la Julian Karangi ambaye alikuwa mwalimu na mmiliki wa shule ya chekechea iliyoko Kibamba.
Shuhuda huyo alisema licha ya tukio hilo la kifo bado wahalifu hao walimkata mkono mama mmoja ambaye alidai hakuweza kulipata jina lake mara moja.
“Tulitoa taarifa polisi hata hivyo, walipofika walikwishaondoka kwa kukimbilia katika pori ambalo halijaendelezwa na mmiliki wake kwa muda mrefu ambapo walitokea kwenye kijiji cha Mpiji ambako waliendelea walivamia nyumba moja moja,”alisema shuhuda huyo.
Aidha, shuhuda huyo alisema marehemu alizikwa juzi Aprili 23 mwaka huu katika kijiji hicho cha Manzese Kibamba wilayani Kinondoni jiji Dar es Salaam.
Alipotafutwa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Christopher Fuime, ili kutoa ufafanuzi kuhusu uvamizi huo, alisema hakuwa na taarifa zozote  kuhusiana na matukio hayo.
“Kama kuna panya road wanaotumia sialaha basi hao siyo panya road bali huo ni ujambazi kwa sababu panya road hawana historia ya kuuwa tangu walipoanza,”alisema Fuime.
Alisema kutokana na mazingingira hayo ya kutumia silaha za moto anafikiri hilo ni kundi lingine kwa hiyo atalifanyia kazi kuanzia sasa na kwamba ameahidi hata kubali kuona uhalifu unaendelea kutokea.
Wakati huo huo Wakazi wa Kimanga wametahadharishwa kwamba wanaweza kufungwa ama kulipishwa faini iwapo watashindwa kutoa michango kwajili ya uslinzi shirikishi iwapo mkutano wa mtaa ukipitisha kulipwa kwa michango hiyo.
Mkuu wa kituo cha Polisi Tabata, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Bakari Goti aliwasihi wananchi kuharakisha michango ambayo itagharamia askari walioandaliwa vinginevyo watakaokaidi kuchanga watafikishwa mahakamani.
Diwani wa Kimanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Kimanga, Manase Mjema amewaonya wananchi wa Kata hiyo juu ya kuweka ngoma za usiku zijulikanazo kama Kigodoro katika sherehe na badala yake wametakiwa kufanya sherehe zao kwenye kumbi.
Akizungumza na wananchi juzi, wakati wa uzinduzi wa kikundi cha Polisi Jamii, Diwani huyo alisema kuwa ngoma hiyo mbali na kuwa kero imekuwa ikisanbaisha watu kuibiwa na kuporwa mali zao kutokana na vijana wahuni kujiiingiza na kuvizia maeneo yaliyo karibu na ngoma hizo.

No comments:

Post a Comment