KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 6 May 2016

BALOZI WA KUWAIT AZINDUA KISIMA CHENYE UREFU WA MITA 90, MTAA WA GOLANI



BALOZI wa Kuwait nchini, Jasem Alnajem, juzi amezindua kisima chenye urefu wa mita 90 kwa ajili ya matumizi ya wakazi wa Mtaa wa Golani, Kimara, Kinondoni jijiini Dar es Salaam.
Mtaa huo wenye wakazi zaidi ya 12,000 unakabiliwa na tatizo la maji, barabara pamoja na huduma nyingine za kijamii tangu ulipoamzishwa miaka nane iliyopita.
Ujenzi wa kisima hicho umefadhiliwa na kikundi cha wahisani kutoka Kuwait, ambao walifikia hatua hiyo baada ya kufahamishwa tatizo hilo na Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea ambaye aliongoza uzinduzi huo.
Katika uzinduzi huo, Balozi huyo alisema baada ya kukamilisha ujenzi huo nchi yake inatarajia kuchimba visima vingine katika mtaa huo ambao ameteuliwa kuwa mlezi wake.
“Baada ya kukamilika mradi huu ni waahidi kuwa huu siyo mwanzo bali tutaendelea kusiriki katika miradi mingine ya maendeleo hususan baada ya mbunge wenu kutujulisha matatizo yenu,”alisema.
Aidha, Alnajem alisema hivi karribuni wataanza ujenzi wa kisima kingine huku akiahidi kumalizia ujenzi wa msikiti ambao umeanza kutokana na michango midogo yaw a umini wa dini ya Kiislamu wa mtaa huo.
Mbunge wa Ubungo Kubenea, aliwaasa wakazi wa mtaa huo kuutumia mradi huo wa maji ili uweze kuwasaidia kwa muda mrefu.
“Nina mawasiliano mazuri na ubalozi huo kwa hiyo niko tayari kufikisha matatizo ya wapiga kura wangu kwa balozi huyu, kila nitakapo yapata baada ya kuhakikishiwa naye kuwa milango iko wazi,”alisema Kubenea.
Bahati Juma, mkazi wa mtaa huo, alisema upatikanaji huduma hiyo ya maji wa shida kwani wamekuwa wakitembea mwendo mrefu kufuata huduma hiyo huku maji ya mifereji ambayo siyo salama kwa afya zao.
“Wakati mwingine tunaletewa maji ya kununua yale mifereji ndoo sh 300 na ya bomb ash 500 kitendo ambacho wakati mwingine baadhi yao wanashindwa kununua kutokana na kukabiliwa na umasikini,”alisema.
Alisema, anaamini kuzinduliwa kwa mradi huo kutasaidia kupunguza tatizo hilo huku wakisubiri miradi mingine mikubwa ya serikali.
Hasan Makamba, alisema kwa vile maji mi moja ya haki za binadamu kwa hiyo wameshukuru kupata kisima hicho kwani kitasaidia kupunguza bajeti kubwa waliyokuwa wakitumia kwa ajili ya kununua maji kila siku.
Mwenyekiti wa Mtaa huo, Laurent Mtoi, alisema mtaa huo uko mpakani mwa wilaya ya Kinondoni na Ilala lakini kutokana na ubovu wa barabara zinazoelekea Kinondoni kunawafanya wakazi wa mtaa huo kukimbilia huduma zote za kijamii katika wilaya ya Ilala.
Kwa hiyo ameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa miundombinu yote yenye masilahi na jamii ikiwemo kukamilisha ujenzi wa shule ambayo hadi sasa vyumba vitano vya madarasa vinahitajika.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment