SERIKALI
ya Mapinduzi Zanzibar imeahidi kuweka mazingira bora yatakayo wezesha sekta
binafsi kuchangia ukuaji wa uchumi waviwanda katika visiwa hivyo.
Waziri
wa Biashara, Viwanda na Masoko, Zanzibar, Amina Salumu Ally, aliyasema hayo
mjini hapo wakati Jumuiya ya Wakulima, Wafanyabiashara na wenye Viwanda ya
Tanzania bara TCCIA na ile ya Zanzibar ZCCIA zilipoingia makubaliano ya
kushirikiana kuendeleza sekta za biashara na viwanda kwa karibu.
Makubaliano
hayo yalitokana na mikutano iliyofanyika awali kwa kuwakutanisha viongozi wa
vyama hivyo, iliyofanyika hivi karibuni.
Alisema
serilikali imefikia hatua hiyo kwa vile inatambua umuhimu wa sekta binafsi
katika kuchangia maendeleo ya biashara na viwanda nchini.
“Nia ya
serikali ya Zanzibar ni kuona Zanzibar ina kuwa ya viwanda na kuifanya inakuwa
kituo kikuu cha kibiashara katika nchi zote za jirani.
“Niwapongeze
kwa hatua mliyofikia kwani imefungua ukurasampya ambao utasidia kukuza biashara
hususan kwa wanawake tena kwa kujianzishiaviwanda vidogovidogo,”alisema Amina.
Aidha, Amina
aliwataka watendaji wa serikali kupunguza urasimu wa katika kukaribisha
wawekezaji wanaotaka kuwekeza Zanzibar kwani endapo wataendelea kuweka vikwazo
visivyo na sababu za kueleweka basi kunaweza kuwakimbiza wawekezaji.
Mkurugenzi
Makazi wa Trade Mark East Afrika, alisema kutiliana saini huko, kutasaidi
kupunguza vikwazo ambavyovilikuwa vikiwakabili wafanyabiashara.
Alisema, kwani kuna wakati baadhi ya wafanyabiashara wa Zanzibar
walikuwa wakikumbwa na changamoto mbalimbali za kufayabiashara zao kutoka
sehemu moja hadi nyingine.
No comments:
Post a Comment