KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday 7 May 2016

WAMACHINGA WA POSTA MPYA NA ZAMANI WATENGWA KUPATIWA MAENEO YAKUFANYIA BIASHARA


MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA, ISAYA MNGURUMI

BAADHI ya wafanyabiashara wadogodogo (Wamachinga), wanaofanya shughuli zao katika eneo la Posta wamelalamikia uwamuzi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Isaya Mngurumi kwa kushindwa kwake kuwapangia eneo la kwenda kufanyia biashara.
Malalamiko yao yanakuja siku mbili baada ya mkurugenzi huyo kutoa agizo la kuwataka wa wafanyabiashara hao kuondoka kwa hiyari yao katika maeneo ambayo siyo rasimi, kuelekea kwenye maeneo yaliyoandaliwa.  
Walisema hayo jijini leo, wafanyabiashara hao,  walishangazwa na uwamuzi wa Mngurumi ambaye wanadai alishindwa kufafanua kwamba wafanyabiashara hao waelekee wapi kuanzia kesho.
Ramadhan Rajab, alisema wamefikia hatua hiyo baada ya kusikia kuwa wanaohusika na utaratibu huo ni wale waliyotambuliwa na kuorodheshwa katika maeneo maalumu.
Alisema, juzi Mngurumi aliyataja maeneo husika kuwa ni  Kariakoo, Karume, Bunguruni, Mombasa, Jangwani, Kibasila, Banana na Gongolamboto.
Wafanyabiashara hao wanatakiwa kwenda kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili yao ambayo ni Kigogo Fresh, Kivule, Soko la Tabata Muslim na eneo lililoko mkabala na gereza la Ukonga.
“Huu utaratibu wa kuwatambua wenzetu ulifanyika lini kwani hatujui siku wala mwaka uliyofanyika wakati ili paswa nasi pia tuorodheshwe kama ilivyokuwa kwa wafanyabiashara wenzetu,”alisema Rajab.
Daniel Khamis, alisema serikali inapaswa kujenga mazingira bora ambayo yatawawezesha vijana kufanyabiashara zao bila ya kuingia kwenye mivutano ambayo inaweza kuwafanya wananchi waichukie serikali yao.
“Tunaomba sehemu na sisi tutengewe eneo kwa vile watakapoanza operesheni ya kuwaomdoa wafanyabiashara katika hayo maeneo ambayo siyo rasmi hata sisi tunahusika lakini ndiyo hatujui tunakwenda wapi,”alisema Khamisi.
Juzi wakati akizungumza na vyombo vya habari, Mngurumi, aliwataka wafanyabiashara hao kuondoka kwa hiyari yao katika maeneo ambayo siyo rasimi hadi jana.
Alisema kwa wale watakaokaidi agizo hilo, hataua kali zitachukuliwa ikiwemo kuchukuliwa bidhaa zao na kupelekwa mahakamani na kupigwa faini.


No comments:

Post a Comment