KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Tuesday 24 May 2016

POLISI KITUO CHA WAZO HILL WALALAMIKIWA



KITUO cha Polisi Wazo Hill jijni Dar es Salaam kimeingia lawamani baada ya kudaiwa kuwaachia watuhumiwa wa makosa ya kugushi nyaraka ili kujimilikisha eneo la ardhi huku wakijua si la kwao. 
Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Mabwepande ambapo watuhumiwa hao walifikishwa kwenye Mahakama ya Ardhi wilayani Kinondoni mwaka 2014 nakubainika kuwa wana kesi ya kujibu. 
Mmiliki halali wa eneo hilo, Samuel Augastino, akizungumza leo, alisema waligushi nyaraka kisha kuuziana wenyewe kinyume cha sheria. 
Aliwataja watu hao kuwa ni Athuman Mnubi, Joseph Mponda na Jacob Pius, ambaye inadaiwa kuwa ni raia wa Msumbiji. 
"Athuman Mnubi akijifanya mmiliki wa eneo hilo lenye ukubwa wa ekari moja na nusu aliliuza kwa sh. 60,000 ambapo mnunuzi alikuwa ni Jacob Pius haya yamefanyika Novemba 25, 1999,"alisema Augastino. 
Alisema baada ya kesi hiyo kendelea kusikilizwa kwa muda mrefu watuhumiwa waliagizwa na Mahakama kupeleka vielelezo vinavyoonesha uhalali wa umiliki wao.
Augastino, alisema baada ya kupeleka vielelezo hivyo, Hakimu aliyekuwa akisikiliza shauri hilo ndipo alipobaini kuwa nyaraka hizo zilizowasilishwa nakamanain zilikuwa za gushi.
"Hakimu alibaini hayo Agosti 13 mwaka jana jambao ambalo alitufahamisha kwamba vielelezo hivyo vilikuwa vya kugushi kwa hiyo akatutaka tuchukue hatua,"alisema Augastino.
Alida kutokana na kitendo hicho hakimu aliwashauri waende polisi kutoa taarifa ili watuhumiwa hao wachukuliwe hatua za kisheria.
Augastino, alisema kweli walifanya hivyo, Agosti 13 mwaka jana, kikatolewa kibali na polisi cha kukamatwa (WH/RB/6812/2015), ambapo walikamatwa kisha kufunguliwa kesi ya kugushi nyaraka. 
Hata hivyo, alidai kuwa baada ya kukamatwa watuhumiwa hao waliachiwa siku iliyofuata bila ya walalamikaji kupewa maelezo ya kuachiwa kwa watuhumiwa hao.
"Tumejaribu mara kadhaa kumuona Mkuu wa Kituo cha Wazo lakini ilishindikana kwani kila tulipofika tuliambiwa hapatikani kitendo ambacho kilitusikitisha na hii imetufanya tukimbilie kwenye vyombo vya habari ili kilio chetu kiwafikie wakubwa mbali waliko,"alisema Augastino.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime, akitolea ufafanuzi malalamiko hayo, aliwashauri walalamikaji hao waende katika kituo hicho kwa ajili ya kumuona  mkuu wa kituo hicho. 
Alimtaka mkuu huyo wa kituo kulishughulikia suala hilo kwa vile liko katika kituo chake na endapo watakosa msaada basi warudi kwake tena hata hivyo, anaaminini kuwa watasaidiwa.

No comments:

Post a Comment