KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Saturday 14 May 2016

WATUMIAJI WA SIMU WAHOJI KUZIMIWA SIMU ZAO KWA MADAI NI BANDIA



BAADHI ya watumiaji wa simu za kiganjani wamepinga uwamuzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwamba ifikapo Juni 30 mwaka huu itazima simu zote bandia zilizoingizwa nchini.
Hivi karibuni TCRA imekaririwa na vyombo vya habari ikiwataka watumiaji wa simu za mkononi kote nchini kuhakikisha simu wanazotumia zinakuwa  na  namba  ya utambulisho  (IMEI NUMBER), kwa lengo la kuzuia wafanyabishara wasio waaminifu kuendelea kuingiza simu bandia nchini.
Wakizungumza jijini Dar es Salaam jana, kwa nyakati tofauti, watumiaji hao walisema wanauhakika mpango huo utakapotekelezwa utaathiri watu wengi wenyekipato cha chini ambao ndiyo wanunuzi wa simu hizo.
Fahdy Juma, alisema hawakubaliani na uwaamuzi huo kwa vile wanaamini kuwa makosa yaliyosababisha wamiliki simu kizo bandia hayawahusu na baadala yake wakuadhibiwa ni wafanyabiashara waliyoziingiza.
“Angalia tangu walipotangaza kwamba watazima simu hizo bandia hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa na serikali ya kuzizuia bado serikali imekuwa ikiwatoza kodi wafanyabiashara hao kwa mizingo ya simu bandia wanazoziingiza nchini,”alisema Juma.
Sikitu Mwanakatwe, alisema tatizo la simu bandia litawaathiri watu wengi wakiwemo wanasiasa, wasomi viongozi wa serikali na wakulima huko vijijini.
Alisema kama wapo wanaonunua simu hizo bandia kwa kukusudia ni sawa lakini kuna wengine wanauziwa baada ya kushawishiwa na wafanyabiashara kwamba ziko kwenye viwango vya kimataifa.
Sikitu, aliishauri mamlaka hiyo kuona kama kuna uwezekano na ikiwapendeza kuachana na mpango huo hiku ikihakikisha kwa kushirikiana na Idara nyingine kuzuia uingizaji wa simu hizo.
Meneja Uhusiano wa TCRA, Innocent Mungi, alisema uzimaji wa simu hizo za bandia uko palepale, kwani zimegundulika kuwa zina madhara makubwa ya kiafya, kiuchumi na kwa ajili ya kulinda usalama wa raia nchini  na Taifa kwa ujumla.
“Unajua simu hizo za bandia hivi sasa hazioani na mfumo wa mawasiliano wa taifa kwa hiyo hata watumiaji wa simu hizo wanapozitumia kihalifu hawawezi kukamatwa kwa hiyo ndiyo maana tunaziondoa sokoni.
“Kuna watu wana masimu ya thamani wenyewe wakijua kuwa yako kwenye viwango kumbe hizo ndiyo baadhi yake ziko kwenye simu bandia ni washauri kwamba wazihakiki huku wakitunza stakabadhi zao siku zikizimwa wakadai fedha zao,waliowauzia  wakikataa wakawashitaki kwa vile kitendo walichofanya ni sawa na wizi,”alisema Mungi.
Mungi, alisema mpango huo siyo wa Tanzania pekee bali imekuwa kushirikiana na baadhi ya taasisi za kimataifa kama vile Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia mawasiliano na shirika la afya duniani ambazi ndizo zilizokubaliana kusitisha matumizi ya simu hizo bandia.

No comments:

Post a Comment