KAMA UNA TUKIO LOLOTE LA KIJAMII, SIASA, UCHUMI TUWASILIANE KWA E-mail: shehesemtawa@gmail.com SIMU: 0719 352 268

Friday 1 July 2016

WAKAZI 65, WA BONDE LA MKWAJUNI WAOMBA MSAADA KWA RAIS MAGUFULI

WAKAZI 65 ambao wamebomolewa nyumba zao katika bonde la Mkwajuni wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, wameiomba serikali ya Rais John Magufuli, iwapatie msaada wa kibinadamu.
Wakazi hao wanahitaji msaada ikiwa ni pamoja na mahitaji ya kijamii kwa vile tangu nyumba zao zilipobomolewa kimakosa ni zaidi ya miezi sita huku wakiishi katika vibanda bila ya msaada wowote kutoka serikalini.
Wakizungumza na wandishi jijini jijini, kwa nyakati tofauti, wakazi hao walisema wamekuwa wakiendelea kuishi katika mazingira hayo magumu, kwa sababu ya kuasubiri uamuzi wa serikali ambayo iliahidi kwa wale waliyokuwa wamejenga kutokana na vibali walivyopewa na maofisa wa serikali wangefidiwa.
Miongoni mwa wakazi hao ni Sabrina Hilal (63), alisema wamefikia hatua hiyo kwa vile wakati nyumba zao zinabomolewa wakazi hao walikuwa na hati halali hivyo kuahidiwa kuwa wangelipwa fidia kwa ajili ya kwenda kuanza maisha mapya sehemu nyingine.
“Tunamuomba Rais Magufuli, atusaidie kwani tunadhani yeye ndiyo mtu wa mwisho ambaye anaweza kutuokoa katika maisha haya magumu kwenye hivi vibanda tunamoishi, atusaidie tuondoke hapa,” alisema Sabrina.
Alisema, tangu opeaheni ya bomoabomoa ya nyumba zilizojengwa katika maeneo ya mabondeni na hatarishi ni zaidi ya miezi sita sasa lakini walipopewa hadi kwamba wangefidiwa hakuna kitingozi yoyote wa serikali aliyewatembelea kuja kujua hatima ya maisha ya wakazi hao.
“Sisi tumebomolewa nyumba zetu lakini tuna hati ambazo tulipewa na Manspaa Kinondoni huku tukilipa hata kodi zaajengo, leo tunashangazwa na ukimnya wa Manispaa yetu”alisema.
Alisema kuwa haki ya kuishi katika vibanda hivyo kumekuwa na madhara makubwa sana ikiwemo watoto kubanwa na kifua kutokana na hali ya hewa ya kipupwe.
Mwanaidi Idd, alisema kwa vile Rais Magufuli ameaikika mara kwa mara nia ya serikali yake ni kusaidia wananchi hivyo anaamini kuwa atalishugulikia suala hilo ili haki ipatikane.
Alisema wanamuomba Rais Magufuli, afanye ziara ya kushtukiza ili kwenda kujionea maisha wanayoishi wananchi wake waliyompigia kura katika uchaguzi mkuu uliyofanyika mwaka jana.

Aidha, Mwanaidi, alishauri serikali kuwachukulia hatua za kishwria kwa maofisa wote wa manispaa ya Kinondoni, ambao walihusika katika utoaji wa vibali vya ujenzi katika maeneo hayo huku wakijua ni hatarishi.

No comments:

Post a Comment